Naam, mie ni ghulamu anayeibuka katika sanaa hii ya utunzi wa mashairi.Bado sijawa malenga hasa bali ningali najaribisha tu katika harakati za kujifunza na kujizoesha uga wenyewe.Sijafuzu bado katika ngoma hii lakini dua yangu ni kuwa, siku moja nitakuwa sogora wa kupigiwa mifano kote katika fani ya utunzi.
Azma yangu ya utunzi ilichipuka nilipokuwa katika kidato cha pili, nikaanza kushiriki mashindano ya utunzi na kukariri mashairi kwenye tamasha ya muziki ya shule za upili.Ingawa sikufika mbali, niliwakisha shule yetu katika mashindano ya wilaya na mkoa wa Nairobi na hii ilinipa ari na motisha ya kuendelea kupiga mbizi katika bahari hii yenye kina kirefu.Sasa hivi, mimi ni mwanagenzi wa maswala ya elimu katika chuo kikuu cha Kenyatta.
Waama, naienzi, naithamini na kuihusudu lugha hii tukufu ya Kiswahili.Kwa yeyote atayepata fursa na satua ya kuyasoma mashairi yangu, nitakuwa na terema sufufu na maridhawa ukichukua nafasi yako kunishauri,kunipongeza, kunielekeza na kunipa changamoto.Kumbuka kinga na kinga ndipo moto uwakapo na daima geza geza mji huwa! TUSAIDIANETUZIDI KUIENZI NA KUIHUSUDU LUGHA HII, KOTE KOTE.
SHUKRANI.
SOLOMON OLE MUSERE.
CHUO KIKUU CHA KENYATTA.
No comments:
Post a Comment